Jinsi ya kupika Kabichi la nyama

Jinsi ya kupika Kabichi la nyama

Mahitaji


  • Nyama ya ngombe 1/2 kilo
  • Vitunguu maji viwili
  • Nyanya nne
  • Pilipili hoho nusu
  • Kabichi 1
  • Viazi vinne
  • Karroti 1
  • Njegere nusu kikombe
  • Mafuta vijiko vitatu vya supu
  • Kitunguu saumu
  • Pilipili manga kiasi
Jinsi ya kutayarisha


  1. Kata nyama,osha,weka chumvi,kitunguu saumu na pilipili manga acha chemsha na uikoroge ili viungo vikolee,ongeza maji kuifunika nyama,acha iive
  2. Kata kabichi kama vile unavyokata la kachumbari lioshe na maji ya vuguvugu,Tayarisha kitunguu,nyanya,karoti,viazi vigawe mara mbili.
  3. Injika chungu jikoni,weka mafuta yapate moto,kaanga kitunguu mpaka kibadilike rangi kiwe hudhurungi,weka nyanya,viazi,supu ya nyama na nyama uloichemsha,acha nyanya iive mpaka ipondeke.Na mchuzi uwe mzito.
  4. Weka carrot na njegere pamoja na kabichi.Acha viendelee kuiva sosi ya kwenye kabichi ikikaribia kukauka weka pilipili hoho acha vichemke dakika kadhaa kisha epua.
  5. Ongezea chumvi ikiwa haijatosheleza
Msosi huu ni mzuri ukiula na wali wa nazi au chapati.Bon apetitt
Previous Post Next Post